Tuesday, February 5, 2013

Na Hamida Khalid, Babati NYUMBA zipatazo 6 zimechomwa moto katika kijiji cha Manyara, kata ya Bagara, Wilaya ya Babati Mkoani Manyara na kuteketezwa kabisa samani zake za ndani pamoja na mifugo wakiwemo mbuzi 64 na kuku zaidi ya 30. Nyumba hizo ambazo zilichomwa moto na wananchi wanaosadikiwa kuwa ni wa kijiji cha jirani cha Bagara kinachopakana na kijiji hicho ni pamoja na nyumba ya Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Barikiely Amsi ambaye pia mifugo yake yote iliteketea. Akiongea na mwananchi katika eneo la tukio Bw. Amsi alieleza kwamba tukio hilo limetokea Februari 3 majira ya jioni ambapo baadhi ya watu wa maeneo hayo wakiwa katika shughuli zao za kujitafutia na yeye na familia yake wakiwa miongoni mwao. Alisema kuwa kilichomshitua kurudi nyumbani kwake alisikia watu wakipiga mayowe kuomba msaada ndipo walipokimbilia eneo hilo na kukuta nyumba sita zilizofuatana zikiwa zinateketea kwa moto. "Wanakijiji tulijitahidi kuzima moto huo tukafanikiwa lakini hakuna kitu hata kimoja tulichofanikiwa kuokoa, wenzangu wameunguliwa vitu vyote vya ndani na mimi pia pamoja na mbuzi 64 na kuku walikuwemo zaidi ya 30, kama mnavyoona hapo mbuzi wanavyomalizikia kuteketea" alisema Bw. Amsi. Aidha Mwenyekiti huyo aliwataja wenzake waliopatwa na mkasa huo kuwa ni pamoja na Bw. Emanuel Halaay, Bw. Shamba Emanuel, Bw. Tiay Nyerere, Bw. Badada Sule na Bw. Maasai Matte. Wakati tukio hilo loikitokea kulikuwepo na baadhi ya wanakijiji ambao walijitambulisha kuwa ni majirani waliopakana na nyumba ya mwenyekiti na kueleza jinsi walivyoona moto ukishika kwenye nyumba hizo na kusema kuwa waliona zikiwaka kwa pamoja. "Wakati moto unawaka nyumba ya nne kutokea hapa kwa mwenyekiti mimi nilikuwepo eneo lile nilipoona moto unawaka nikasogea karibu, nikagundua ni nyumba inaungua ndipo nikaanza kukimbia ili kuita wenzangu, wakati nakuja huku nikaona na nyumba zinazofuata nazo zinaungua ndipo nikapiga yowe kuomba msaada" alisema Bw. Banga Bura ambaye ni jirani wa Bw. Amsi. Kwa upande wake Mtendaji wa kijiji hicho Bi. Selina Emanuel alisema kuwa wakati tukio hilo linatokea alikuwepo nyumbani kwake ambapo ni mbali kidogo na eneo la tukio hivyo alichelewa kufika na kukuta tayari nyumba zimekwishateketea. "Kwakweli mimi sina hata cha kuelezea kwakuwa sikuwepo eneo la tukio, nilipata taarifa kwa njia ya simu hivyo wakati najiandaa kuja polisi walishafika na tayari mtu mmoja ameshakamatwa yuko mikononi mwa polisi kuhusiana na tukio hilo" alifafanua Mtendaji huyo. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara Bw. Akili Mpwapwa alisema kuwa watu wawili wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo kupitia kwa wasiri wa polisi waliokuwepo katika eneo hilo. Kamanda Mpwapwa aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Marco Alli (42) na Iddi Athumani (27) wote wkulima na wakazi wa kijiji cha Magara na kubainisha kwamba chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mpaka kati ya kijiji cha Manyara na kijiji cha Magara. Mwisho.

Monday, June 25, 2012

SISI TUTAIJENGA TANGA

Kufuatia ujenzi wa barabara ya Segera- Tanga, baadhi ya Wadau wametoa maoni yao kuhusu ubovu uliokuwepo katika barabara hiyo na huu unaoendelea katika barabara ya kutokea Himo-Segera. Barabara hiyo ni mbovu na imekuwa ikimeguka kila kukicha, kwa wengi walio wagonjwa hasa ambao magonjwa yao hayaendani na ubovu wa barabara wamekuwa wakihoji ni lini itapatiwa ufumbuzi angalau wa kuziba viraka tu. Tuanze kuwakumbusha Wabunge wetu juu ya ahadi zao walizozitoa kipindi kile cha kampeni kuhusu barabara zetu kwani inaonekana kidogo wameanza kujisahau.
Posting from an internet training with journalists in Arusha, Tanzania, 2010

Tuesday, February 22, 2011

MUAFAKA WA JANGA HILI NI LINI?

Poleni sana ndugu zetu Wahanga wa Mabomu huko Jijini, kwa mara nyingine tena janga la mabomu limeendelea kutesa familia lukuki katika nchi yetu.

Hivi ni kweli Wananchi tutakuwa na makosa gain pindi tutakapohoji kuhusiana na mauaji haya yasiyo na kificho kwa ndugu zetu? Naomba mnisaidie mimi kwa upeo wangu huu mdogo kuhusiana na hili….

Bado tuko pembezoni mwa ulimwengu huu tukiangalia na kutegesha macho na masikio yetu japo tupate kusikia kauli nzuri zitakazoturidhisha kwa hili ….Hivi ni kweli inawezekana kuwa ni bahati mbaya au ni Rehema ya Mungu kwamba yeye aliyeimba nchi na Dunia ndiye hasa anayesababisha kulipuka kwa mabomu Ardhini?

Naomba mnisaidie hili kwani kwa sasa walio wengi kama mimi tunasubiri tena kwa mara ya tatu kusikia kama ni zamu ya Mabibo au wapi…….

Kwa tahadhari za namna hii itakuwa saf sana kwani watu wanaweza kujiandaa kuhama makazi yao kwa hiari kuliko kuendelea kusubiria vifo visivyotamanika…….NATOA POLE YA DHATI KABISA KWA NDUGU WOTE WA MAREHEMU NA WALIOATHIRIKA NAMI NIKIWA MMOJAWAO..

Monday, January 31, 2011

KWA WALE WOTE WANAOGUSWA NA MAFANIKIO YALIYOPATIKANA AU YASIYOPATIKANA KATIKA KIPINDI CHA MADARAKA YA JK KUANZIA 2005-2010

Kushiriki kwako katika mchakato huu ndiko kutakakofanya Watanzania walio wengi kujua haki zao kimsingi katika kuziboimarisha kuziboresha katika kipindi kilichopita ndani ya madaraka ya Mheshimiwa JK..Tutakuwepo baada ya muda kukupa live………………..

Friday, November 19, 2010

Thanksfull to MISA-Tanzania

Today October 19 we are finish our training which we have started since October 15 in Arusha, this training is about to learn the Internet in morden journalism and its joined the Journalists from four Regions which is Arusha,Kilimanjaro,Tanga and Manyara.

We are learned more for fact-finding, news monitoring, communication and publication and also we wouldpractise how to search for information through the internet and how to publish journalistic content online.

I thanks for MISA- Tanzania for getting this training because it make me in another thinking about how can inter in deeply to search for information through the Internet.

Mmmh.... huu uchakachuaji mwengine umezidi...yaani nyomi lote hili lakini matokeo yake!!!! haya mwaya lakini mwenyewe hajaridhika nayo...







Hivi kweli unaweza kumuiga huyu? Watoto wake wanamchukulia ni Mama mwema lakini sijui kama wanaweza kumuiga katika staili hii.

Sijui kama unaweza kutambua hii inayochezwa hapa ni ngoma ya kabila gani Tanzania hii?

Baadhi ya Waandishi wa Habari walioshiriki kwenye semina ya kujifunza jinsi ya kutumia Internet kwa ufasaha ambayo ilifanyika Mkoani Arusha. Semina hiyo iliwashirikisha Wana habari kutoka kanda ya kaskazini, Mikoa ya Arush, Kilimanjaro, Tanga na Manyara ambapo iliandaliwa na MISA-Tanzania.





Kipindi cha kampeni walikuwa wakiwa pamoja kwenye majukwaa pamoja na tofauti zao.


Walisema Mafahari wawili hawakai zizi moja, waone kama sio wale wa kwenye majukwaa

Ni siasa au Gulio

Bado wapo wapo kwanza


Wednesday, November 17, 2010

The 3rd Day

Todays lesson wednesday (17) nov. 2010, we have make a long practicle about how to use the google with finding the diferents websites like www.freemedia.co.tz http://www.internetworldstats.com/stats1.htm and out of this also we make an exercise about how to use that while we want to find another program like emails with using the google.

And that we are make sure that every one who getting this training will know well how to use internet and another program like that and must be her/his blogger.

Nov 17th, Eidd Mubarrak 4 all Islamic.

Eidd is a wonderfull DAY
2Pray,
2Love,
2Care,
2Smile, 2Celebrate &
2Thanks Allah 4 all……

Eidd Mubarrak..

Nawatakia kila la kheri wale Waislamu woote duniani kote
walioungana kula Eidd siku ya leo……Eidd Mubarrak..

Tuesday, November 16, 2010

The 2nd Day

In short I can said am understood in such about todays subject especially to inter in the glob, yet am very happy to say congratulation and thanksfull to Misa Tanzania for care the Journalists about this training of Internet.

arusha

Posting from an internet training with journalists in Arusha, Tanzania, 2010

arusha

Posting from an internet training with journalists in Arusha, Tanzania, 2010
Posting from an internet training with journalists in Arusha, Tanzania, 2010